Friday, May 06, 2016

RAIS MAGUFULI AWAONYA WALIOFICHA SUKARI,ATISHIA KUICHUKUA SUKARI HIYO NA KUIGAWA BURE KWA WANANCHI


Rais Dkt.John Pombe  Magufuli amewaonya aalioficha Sukari na kutishia  Kuichukua Sukari hiyo na Kuigawa Bure Kwa Wananchi.Rais Magufuli ametoa onyo kali kwa wafanyabiashara walioficha sukari ili baadae waiuze kwa bei  ya juu.

Amesema wafanyabiashara hao wenye tamaa ya pesa walikuwa wakifuata sukari iliyo Expire huko Brazili   na kuileta nchini ili watengeneze faida na ndo maana serikali iliwapiga marufuku kuagiza.Rais Magufuli ameyasema hayo  wakati akiwasalimia wananchi wa Katesh, Mkoani Manyara. Rais ametoka Mkoani Dodoma , anaelekea Mkoani Arusha kwa usafiri wa gari.

Akiongea na mamia ya wananchi hao waliojitokeza kumlaki njiani, Rais Magufuli amewatoa hofu wananchi kuhusu uhaba wa sukari kwa kuwa tayari wako  katika mchakato wa kuagiza makontena ya sukari nje ya nchi ili kuwakabili wafanyabiashara walioficha bidhaa hiyo.Amesema kwa taarifa alizonazo kuna mfanyabiashara alienda akanunua sukari pale Kilombero zaidi ya tani 3000 na hataki kuzichukua 
Pia amesema kuna mwingine ana godauni huko Mbagala yenye tani 4000  ambazo hataki kuzitoa ili wananchi wakose sukari.Rais Magufuli amesema ameviagiza vyombo vya dola viwafuatilie ili ikithibitika sukari waliificha basi ichukuliwe na kugawiwa bure kwa wananchi na pia watapigwa marufuku kufanya biashara yoyote hapa nchini

No comments:

Post a Comment