Tuesday, April 12, 2016

KONGAMANO LA UWAJIBIKAJI KWA WADAU WA SEKTA YA MAFUTA NA GESI.

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.Philip Mpango akizungumza na wadau  (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa Kongamano la uwajibikaji katika sekta ya Mafuta na Gesi lililoandaliwa na taasisi ya WAJIBU – Institute of Public Accountability  Aprili 11,2016 jijini Dar es Salaam.



Mkurugenzi wa Taasisi ya WAJIBU – Institute of Public Accountability Bw.Ludovick Utouh akizungumza na wadau waliyoshiriki Kongamano linalohusu uwajibikaji katika sekta ya Mafuta na Gesi (hawapo pichani)  kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.Philip Mpango (kulia) akikata utepe kuashiria ufunguzi  rasmi  wa Taasisi ya WAJIBU – Institute of Public Accountability na (kushoto) ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Bw.Ludovick Utouh,sherehe hizo zimefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau waliyoshiriki Kongamano linahusu Uwajibikaji katika sekta ya Gesi na Mafuta wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na  Mkurugenzi wa Taasisi ya TWAWEZA Bw.Aidan Eyakuze (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo lililofanyika  jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (wanne kushoto)akiwa katika picha ya pamoja na wadau waliyoshiriki Kongamano la Uwajibikaji katika sekta ya Mafuta na Gesi,(watatu kulia ni)aliyekuwa  Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na (watatu kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya WAJIBU – Institute of Public Accountability Bw.Ludovick Utouh.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya WAJIBU – Institute of Public Accountability Bw.Ludovick Utouh wakiwa wanaonyesha kibao kinachoonyesha ufunguzi rasmi wa taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment