Friday, January 15, 2016

UJENZI WA SHULE NI JUKUMU LA WADAU MBALIMBALI KUSHIRIKI KATIKA KUKAMILISHA SUALA HILO.

Na Anaseli Stanley,
Mkuu wa wilaya ya kinondoni bw. Paul Makonda amewataka wadau na makampuni mbalimbali kuendelea kusaidia azimio la ujenzi wa shule saba katika wilaya hiyo kwa lengo la kusaidia watoto zaidi ya elfu 3 ambao wana uhitaji wa elimu ya sekondari.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini dare s salaam wakati akipokea misaada hiyo Bw. Makonda amesema kuwa anawashukuru wadau hao na kuwataka wengine kujitokeza kusaidia kukamilisha kwa zoezi hilo la ujenzi

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI, PROF. SOSPETER MUHONGO AMEIAIGIZA KAMPUNI YA UENDELEZAJI JOTOARDHI TANZANIA (TGDC LTD) KUWA IFIKAPO JUNE 2016, IWE IMEANZA KUCHORONGA MASHIMO 3 KATIKA ENEO LA ZIWA NGOZI.

WAZIRI wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo ameiaigiza  Kampuni ya Uendelezaji Jotoardhi  Tanzania (TGDC Ltd) kuwa ifikapo June 2016, iwe imeanza kuchoronga mashimo 3 katika eneo la Ziwa Ngozi ikiwa ni hatua ya mwisho inayohitajika kabla ya kuanza kujenga mitambo ya kuzalisha jotoardhi.

WATU WENYE ULEMAVU WA NGOZI WANATARAJIA KUFANYA UZINDUZI WA STIKA MAALUM JANUARI 26,

Na Nyakongo Manyama-MAELEZO
TAASISI ya  watu wenye ulemavu wa ngozi mkoa wa Dar es salaam inatarajia kufanya uzinduzi wa  ‘stika’ maalum yenye ujumbe wa kutokomeza mauaji ya watu wenye albinism utakaofanyika januari 26 mwaka huu.Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa taasisi hiyo Bw. Michael Lugendo amesema kuwa uzinduzi huo utafanyika katika kituo cha polisi kati jijini Dar es Salaam kuanzia saa tano asubuhi.

HUDUMA ZA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA HAPA NCHINI ZIMEKUMBWA NA CHANGAMOTO MBALIMBALI IKIWEPO NA WATOA HUDUMA WASIOZINGATIA SHERIA, KANUNI NA MIONGOZO MBALIMBALI.


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, 
JINSIA, WAZEE NA WATOTO
MAELEZO YA WAZIRI KUHUSU TIBA ASILI NA TIBA MBADALA
 
Ndugu Wananchi, Katika nchi yoyote ile uhuru usio na mipaka ni jambo la hatari; lakini pia hakuna haki isiyo na wajibu. Vivyo hivyo, katika huduma za Tiba Asili na Tiba Mbadala hapa nchini kuna Sheria, Kanuni na Taratibu za Maadili zinazoweka masharti, uhuru na mipaka; pia haki na wajibu wa kila mdau. 

Huduma za tiba asili na tiba mbadala ni huduma zinazotambulika na Jamhuri yetu, watu wake na ina thamani kubwa. Aidha, ni huduma inayotambuliwa na sayansi ya tiba ya kisasa. Hata hivyo huduma hizo zimekumbwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa watoa huduma wasiozingatia Sheria, Kanuni na Miongozo mbalimbali. 

SERIKALI IMEWATAKA WAWEKEZAJI WA TANZANIA KUUNGANA NA WAWEKEZAJI WA KIMATAIFA KUINUA WIGO NA KUJENGA UZOEFU

Na, Anaseli Stanley.
Serikali imewataka wawekezaji wa Tanzania waungane na wawekezaji wa mataifa mbalimbali kwa lengo la kupata uzoefu na kufanya kazi nyingi za serikali hapa nchini ili makampuni ya Tanzania yawe na uwezo wa kutenda kazi kubwa na kuongeza kipato kwa taifa. 

Hayo yameelezwa mbele ya waandishi wa habari jijin dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa wakandarasi wa japani na watanzania wazziri mkuu MH.Kasim Majaliwa amesema kuungana huku kutsaidia kubadilishana mawazo na kujadili namna mbalimbali za uendeshaji wa makampuni ya ndanina kuongeza ushindani na mataifa mengine.

Wednesday, January 13, 2016

MAHABUSU YA WATOTO JIJINI DAR ES SALAAM YAPEWA VITU MBALIMBALI NA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA

 Afisa Mfawidhi wa Mahabusu ya Watoto ya jijini Dar es salaam Bw. Ramadhan Yahaya (kulia) akipakua msaada wa vyakula na vitu mbalimbali vilivyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania leo jijini Dar es salaam. Anayeshuhudia kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Mahakama Kuu ya Tanzania Bw. Nurdin Ndimbe
 Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Mahakama Kuu ya Tanzania Bw.

WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU WANAOSOMA KATIKA VYUO MBALIMBALI KWA MWAKA WA MASOMO 2015 NA 2016 WAKUMBUKWA NA BODI YA MIKOPO.

Na Jesca Mathew na Anaseli Stanley.
Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu imetoa jumla ya sh  bilioni 459 fedha za kitanzania  kwa wanafunzi wa elimu ya juu 122,486 wanaosoma katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi katika mwaka wa masomo 2015/2016.
Hayo yameelezwa na meneja wa habari, elimu na mawasiliano Omega Ngole amesema kuwa hiyo ni idadi kubwa ya wanafunzi walionufaika na mkopo huo tangu kuanzishwa kwa bodi mwezi julai 2005.
‘’Katika mwaka uliopita wa masomo 2014/2015 serikali kupitia bodi ilitoa jumla ya tsh bilioni 341 ziliwanufaisha wanafunzi 99,069 alisema’’.