WAZIRI wa
Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo ameiaigiza Kampuni ya
Uendelezaji Jotoardhi Tanzania (TGDC Ltd) kuwa ifikapo June 2016, iwe
imeanza kuchoronga mashimo 3 katika eneo la Ziwa Ngozi ikiwa ni hatua ya mwisho
inayohitajika kabla ya kuanza kujenga mitambo ya kuzalisha jotoardhi.
