Na Nyakongo Manyama-MAELEZO
TAASISI ya watu wenye ulemavu wa
ngozi mkoa wa Dar es salaam inatarajia kufanya uzinduzi wa ‘stika’ maalum
yenye ujumbe wa kutokomeza mauaji ya watu wenye albinism utakaofanyika januari
26 mwaka huu.Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,
Mkurugenzi wa taasisi hiyo Bw. Michael Lugendo amesema kuwa uzinduzi huo
utafanyika katika kituo cha polisi kati jijini Dar es Salaam kuanzia saa tano
asubuhi.
