Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu imetoa jumla
ya sh bilioni 459 fedha za kitanzania kwa wanafunzi wa elimu ya juu 122,486
wanaosoma katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi katika mwaka wa masomo
2015/2016.
Hayo yameelezwa na meneja wa habari, elimu na mawasiliano
Omega Ngole amesema kuwa hiyo ni idadi kubwa ya wanafunzi walionufaika na mkopo
huo tangu kuanzishwa kwa bodi mwezi julai 2005.
‘’Katika mwaka uliopita wa masomo 2014/2015 serikali
kupitia bodi ilitoa jumla ya tsh bilioni 341 ziliwanufaisha wanafunzi 99,069
alisema’’.