Wednesday, January 13, 2016

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AFIKA NA KUFARIJI FAMILIA YA BABA WA TAIFA KUFUATIA MSIBA WA MBUNGE WA ZAMANI CHADEMA LETICIA NYERERE NA PIA KUMTEMBELEA WAZIRI MKUU WA AWAMU YA TATU MHE.SUMAYE KATIKA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI.

 Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akitia saini kitabu cha Maombolezo ya kifo cha Mbunge wa zamani,Leticia mageni Nyerere wakati alipokwenda kumhani mjane wa Baba wa taifa, Mama Maria Nyerere Msasani jijini Dar es salaam Januari 12, 2016. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

Monday, January 11, 2016

KWA MUJIBU WA KATIBU MKUU WA CHAMA CHA WANANCHI CUF MAALIM SEIF HAMAD AMESEMA KURUDIWA UCHAGUZI ZANZIBAR ITASABABISHA MACHAFUKO VISIWANI HUMO.

Aliyekuwa mgombea urais Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amesema kuwa kutokana na mgogoro wa kisiasa unaoendelea visiwani humo usipopatiwa ufumbuzi mara moja na kulazimisha kuwa uchaguzi huo urudiwe nidhahiri kuwa hatua hiyo inalazimisha kuwepo kwa hali ya machafuko visiwani humo.

Saturday, January 09, 2016

TAARIFA YA SERIKALI KUHUSU ZOEZI LA KUHAMISHA WAKAZI WA MABONDENI KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM




Utangulizi
Nchi yetu ina kingo za mito na mabonde na maeneo mengi hatarishi ambamo watu wanaishi kinyume cha sheria, huku wakiharibu mazingira na kuhatarisha maisha yao.  Kutokana na uhaba wa makazi, hali ni mbaya zaidi katika mabonde ya Jiji la Dar es Salaam, hasa bonde la Mto Msimbazi.

ASKOFU MKUU WA JIMBO KUU LA KATOLIKI LA DAR ES SALAAM, MWADHAMA POLYCARP KARDINALI PENGO AMEPONGEZA WELEDI WA HUDUMA YA TASISI YA MOYO ILIYOPO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI.

Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kupongeza jopo la Madaktari waliomhudumia katika Hospitali ya Mhimbili.

Friday, January 08, 2016

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU VIKAO VYA TATHMINI NA UCHAMBUZI VYA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)



Katika utaratibu wake wa kujipanga na kuendelea kutekeleza mikakati ya malengo ya muda mfupi na muda mrefu kwa ajili ya kufikia lengo kuu la kushinda uchaguzi, kushika dola na kuongoza serikali kwa ajili ya kuwatumikia wananchi, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekuwa na utamaduni wa kuwa na vikao vya kujitathmini na kufanya uchambuzi kila baada ya uchaguzi mkuu na kuweka mpango kazi unaopaswa kutekelezwa na chama kwa miaka mitano inayofuata.

PICHA RASMI YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI INAPATIKANA IDARA HABARI MAELEZO KWA SHILINGI 15,000.



Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari Maelezo Bi Zamaradi Kawawa akionesha kwa  waandishi wa Habari  picha rasmi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt John Pombe Joseph Magufuli,kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO  Bw. Raphael Hokororo.picha hiyo inauzwa sh. 15,000/- tu.