Showing posts with label Tumaini Makene. Show all posts
Showing posts with label Tumaini Makene. Show all posts

Friday, January 08, 2016

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU VIKAO VYA TATHMINI NA UCHAMBUZI VYA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)



Katika utaratibu wake wa kujipanga na kuendelea kutekeleza mikakati ya malengo ya muda mfupi na muda mrefu kwa ajili ya kufikia lengo kuu la kushinda uchaguzi, kushika dola na kuongoza serikali kwa ajili ya kuwatumikia wananchi, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekuwa na utamaduni wa kuwa na vikao vya kujitathmini na kufanya uchambuzi kila baada ya uchaguzi mkuu na kuweka mpango kazi unaopaswa kutekelezwa na chama kwa miaka mitano inayofuata.