Nchi yetu ina kingo za mito na
mabonde na maeneo mengi hatarishi ambamo watu wanaishi kinyume cha sheria, huku
wakiharibu mazingira na kuhatarisha maisha yao. Kutokana na uhaba wa
makazi, hali ni mbaya zaidi katika mabonde ya Jiji la Dar es Salaam, hasa bonde
la Mto Msimbazi.
