Katika
utaratibu wake wa kujipanga na kuendelea kutekeleza mikakati ya malengo ya muda
mfupi na muda mrefu kwa ajili ya kufikia lengo kuu la kushinda uchaguzi,
kushika dola na kuongoza serikali kwa ajili ya kuwatumikia wananchi, Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekuwa na utamaduni wa kuwa na vikao vya
kujitathmini na kufanya uchambuzi kila baada ya uchaguzi mkuu na kuweka mpango
kazi unaopaswa kutekelezwa na chama kwa miaka mitano inayofuata.