Showing posts with label Ummy Mwalimu. Show all posts
Showing posts with label Ummy Mwalimu. Show all posts
Thursday, March 16, 2017
UMMY MWALIMU ATOA MIEZI MITATU KUANZISHWA DUKA LA DAWA
Friday, April 08, 2016
WAZIRI UMMY MWALIMU AZINDUA DUKA LA DAWA LA MSD KANDA YA MBEYA.
Na Rabi Hume.
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amefanya uzinduzi wa duka la dawa la Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kwa Kanda ya Mbeya.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Waziri Mwalimu amesema uzinduzi wa duka hilo ni sehemu ya jitihada zinazofanywa na serikali ya Rais Magufuli kuwatia wananchi huduma bora na kwa gharama nafuu.
“Neema hii imekuja kwa kipindi cha Rais Magufuli, sasa amekidhi matakwa na shauku ya wananchi wa Mbeya kwa kuwapa duka la dawa.
“Sera ya huduma ya afya inataka wananchi wachangie isipokuwa wazee, watoto na wajawazito na kupitia duka hili wananchi wataweza kupata dawa kwa gharama nafuu,” amesema Mhe. Mwalimu.
Duka hilo la dawa la Kanda ya Mbeya limetumia Shilingi Milioni 13 kwa ukarabati wa jingo na vifaa vyake.
Ummy Mwalimu akionesha moja ya dawa inayouzwa dukani hapo kwa shilingi 7,000 ambapo kwenye maduka binafsi inauzwa shilingi 25,000,kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurine Bwanakunu na kulia ni Mfamasia wa duka hilo, Cornel Mkeng'e
Saturday, January 09, 2016
ASKOFU MKUU WA JIMBO KUU LA KATOLIKI LA DAR ES SALAAM, MWADHAMA POLYCARP KARDINALI PENGO AMEPONGEZA WELEDI WA HUDUMA YA TASISI YA MOYO ILIYOPO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI.
Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kupongeza jopo la
Madaktari waliomhudumia katika Hospitali ya Mhimbili.
Subscribe to:
Posts (Atom)
