Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (katikati), akipata taarifa ya maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa Mtwara kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), mkoani humo, Bi. Zitta Majinge (kulia), mara baada ya kuwasili leo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Bw. Evod Mmanda.
Showing posts with label Waziri wa Ujenzi. Show all posts
Showing posts with label Waziri wa Ujenzi. Show all posts
Thursday, February 16, 2017
PROF. MBARAWA: UWANJA WA NDEGE WA MTWARA UJENZI MWEZI JULAI
Monday, October 03, 2016
WAZIRI PROF. MBARAWA AITAKA TTCL KUTAFUTA WATEJA.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akiangalia taarifa zinazoingia katika mfumo wa kuhifadhi kumbukumbu alipofanya ziara ya kushtukiza katika Kituo mahiri cha kuhifadhi Kumbukumbu cha Taifa (Internet Data Centre), kilichopo eneo la Kijitonyama jijini Dar es salaam.
Monday, September 26, 2016
Friday, September 23, 2016
WABUNIFU MAJENGO NA WAKADIRIAJI MAJENZI WAASWA KUUNGANA
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amezungumzia umuhimu wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi kuungana ili waweze kupata fursa katika miradi mikubwa ya ujenzi itakayoanza hivi karibuni hapa nchini.
Tuesday, August 30, 2016
WAZIRI MBARAWA AFUNGUA KOZI MPYA YA MAFUNZO YA WAKUFUNZI WA MARUBANI
Rubani Focus Mmbaga kutoka Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), akitoa maelezo ya namna ndege inavyoendeshwa kwa kutumia kifaa maalum cha mafunzo ya urubani (simulator) kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya wakufunzi wa marubani uliofanyika jijini Dar es salaam.
Wednesday, August 03, 2016
MKANDARASI APEWA WIKI MBILI KURUDISHA VIFAA NA KUENDELEA NA UJENZI
Mbunge wa Jimbo la Nkasi kaskazini Mhe. Ally Kessy (mwenye kofia) akieleza jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati alipokagua miundombinu ya Bandari ya Kipili, Mkoa wa Rukwa.
Wednesday, July 20, 2016
Saturday, July 16, 2016
Tuesday, July 12, 2016
WAZIRI MBARAWA ARIDHISHWA NA KASI YA UPANUZI WA UWANJA WA UWANJA WA NDEGE, DODOMA
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ameridhishwa na maendeleo ya upanuzi wa uwanja wa ndege wa Dodoma ambapo mpaka sasa ujenzi huo umefikia asilimia 35 ikiwa ni kazi iliyotekelezwa ndani ya siku 18 toka alipotoa agizo hilo mwishoni mwa mwezi juni mwaka huu.
Ametoa kauli hiyo alipokuwa akikagua ujenzi wa uwanja huo na kumhimiza mkandarasi wa Kampuni ya Chico kuendeleza kasi ya ujenzi huo ili kukamilisha kwa wakati uliopangwa na kutoa msisitizo kwa makandarasi wengine wanaotekeleza miradi mbalimbali nchini kujipanga na kufanya kazi kwa ushirikiano ili kukamilisha miradi hiyo kwa muda mfupi kulingana na makubaliano ya mikataba.
PROFESA MBARAWA AFUNGUA SEMINA YA KIMATAIFA YA WADAU WA BARABARA, AWATAKA KUJIELIMISHA HUKUSU MFUMO MPYA WA UJENZI WA BARABARA.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua rasmi semina ya wadau wa barabara mjini Arusha.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akifafanua jambo wakati wa ufunguzi wa semina ya wadau wa barabara iliyoanza mjini Arusha.
Friday, May 27, 2016
WAZIRI PROFESA MAKAME ATEMBELEA DARAJA LA NYERERE NA KITUO CHA KUPIMIA MAFUTA YAINGIAYO NCHINI KUONA MAENDELEO
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiongea na wawakilishi wa kampuni ya Mabey Bridge kutoka Marekani(hawapo pichani) na wadau wengine wa Ujenzi leo kuhusu mpango wa kujenga fly overs takribani tatu katika jiji la Dar es salaamu kwa lengo la kupunguza msongamano wa magari katika jiji.
Wednesday, April 06, 2016
WAZIRI PROF. MBARAWA AKAGUA DARAJA LA RUSUMO NA VITUO VYA PAMOJA VYA FORODHA KABLA YA UFUNGUZI:
Muonekano wa barabara ya Nyakahura-Rusumo inayounganisha Tanzania na Rwanda kupitia Daraja la Rusumo wilayani Ngara.
Mtaalam kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wa pili kulia akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa tatu kulia), alipotembelea ofisi hizo katika Kituo cha pamoja cha forodha (One Stop Border Post) upande wa Tanzania kilichopo Rusumo wilayani Ngara, wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Sekta ya Ujenzi Eng. Joseph Nyamhanga.
Wednesday, March 16, 2016
DARAJA LA KIGAMBONI JIJINI DAR ES SALAAM KUFUNGULIWA RASMI MWEZI WA NNE:
Sunday, March 13, 2016
MBARAWA AFUNGUA RASMI SAFARI ZA TRENI RELI YA KATI KATIKA ENEO LA KIDETE, WILAYANI KILOSA,
Muonekano wa Sehemu ya Reli katika eneo la Kidete, Wilayani Kilosa, mara baada ya ukarabati kufuatia mvua kubwa zilizonyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma na kukata Mawasiliano kati ya Mkoa wa Morogoro na Dodoma.
Kazi za ukarabati wa mwisho zikiendelea katika eneo la Kidete, Wilayani Kilosa, mara baada ya ukarabati kufuatia mvua kubwa zilizonyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma na kukata Mawasiliano kati ya Mkoa wa Morogoro na Dodoma.
Treni ya Mizigo ikiwa tayari kuanza safari katika eneo la Kidete Wilayani Kilosa, kufuatia kukamilika kwa ukarabati wa eneo hilo, uliodumu kwa takriban miezi miwili na hivyo kurudisha mawasiliano ya reli kati ya Mkoa wa Morogoro na Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Mhandisi wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO), Mhandisi Felix Nlalio, kuhusu namna ya kudhibiti mkondo wa maji katika mto mkondoa yasiathiri hifadhi ya reli.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akikagua bwawa la Kidete linaloelezwa kuathiri hifadhi ya reli katika stesheni za Mzaganza, Munisagara, Kidete na Magulu Wilayani Kilosa.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa viongozi wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), kuhusu namna ya kushirikisha wananchi kulinda hifadhi ya reli.
Subscribe to:
Posts (Atom)



