Showing posts with label uchukuzi na mawasiliano. Show all posts
Showing posts with label uchukuzi na mawasiliano. Show all posts

Thursday, February 16, 2017

PROF. MBARAWA: UWANJA WA NDEGE WA MTWARA UJENZI MWEZI JULAI

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (katikati), akipata taarifa ya maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa Mtwara kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), mkoani humo, Bi. Zitta Majinge (kulia), mara baada ya kuwasili leo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Bw. Evod Mmanda.

Monday, October 03, 2016

WAZIRI PROF. MBARAWA AITAKA TTCL KUTAFUTA WATEJA.

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akiangalia taarifa zinazoingia katika mfumo wa kuhifadhi kumbukumbu alipofanya ziara ya kushtukiza katika Kituo mahiri cha kuhifadhi Kumbukumbu cha Taifa (Internet Data Centre), kilichopo eneo la Kijitonyama jijini Dar es salaam. 

Wednesday, March 16, 2016

DARAJA LA KIGAMBONI JIJINI DAR ES SALAAM KUFUNGULIWA RASMI MWEZI WA NNE:

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akipata maelezo kutoka kwa Meneja Msimamizi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni Eng. Karim Mattaka alipokagua daraja hilo leo jijini Dar es salaam.
 Mwonekano wa daraja la Kigamboni ambalo litafunguliwa rasmi mwezi ujao.
Barabara za maingilio (inter change) ya Daraja la Kigamboni upande wa Kurasini.

Sunday, March 13, 2016

MBARAWA AFUNGUA RASMI SAFARI ZA TRENI RELI YA KATI KATIKA ENEO LA KIDETE, WILAYANI KILOSA,

Muonekano wa Sehemu ya Reli katika eneo la Kidete, Wilayani Kilosa, mara baada ya ukarabati kufuatia mvua kubwa zilizonyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma na kukata Mawasiliano kati ya Mkoa wa Morogoro na Dodoma.

Kazi za ukarabati wa mwisho zikiendelea katika eneo la Kidete, Wilayani Kilosa, mara baada ya ukarabati kufuatia mvua kubwa zilizonyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma na kukata Mawasiliano kati ya Mkoa wa Morogoro na Dodoma.
Treni ya Mizigo ikiwa tayari kuanza safari katika eneo la Kidete Wilayani Kilosa, kufuatia kukamilika kwa ukarabati wa eneo hilo, uliodumu kwa takriban miezi miwili na hivyo kurudisha mawasiliano ya reli kati ya Mkoa wa Morogoro na Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Mhandisi wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO), Mhandisi Felix Nlalio, kuhusu namna ya kudhibiti mkondo wa maji katika mto mkondoa yasiathiri hifadhi ya reli.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akikagua bwawa la Kidete linaloelezwa kuathiri hifadhi ya reli katika stesheni za Mzaganza, Munisagara, Kidete na Magulu Wilayani Kilosa.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa viongozi wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), kuhusu namna ya kushirikisha wananchi kulinda hifadhi ya reli.

Thursday, January 28, 2016

SERIKALI YA TANZANIA KUAHIDI KUJENGA BARABARA KWA KIWANGO CHA LAMI.

Serikali imeahidi kuendelea na ujenzi wa barabara katika maeneo tofauti nchini kwa kiwango cha lami ili kutatua adha kubwa ya ubovu wa barabara ulipo katika maeneo mengi nchini.

Hayo yamesemwa leo Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano  Mhe. Eng Godwin Ngonyani akijibu maswali ya wabunge waliouliza kuhusu mpango wa serikali kuboresha barabara zilizopo na kujenga mpya ili kukabiliana na adha ya ubovu wa barabara nchini.

Thursday, January 21, 2016

SHIRIKA LA POSTA TANZANIA (TPC) LAAGIZA MAPATO YAKUSANYWE KWA NJIA YA YA ELEKTRONIKI.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora alifanya ziara ya kutembelea Shirika la Posta Tanzania ili kufahamu utendaji kazi na utekelezaji wa majukumu ya Shirika.