Thursday, October 06, 2016

UMASKINI NI MATOKEO YA MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA YANAYOAMBATANA NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

Na Barnabas Kisengi,
IMEELEZWA kuwa Matumizi mabaya ya madaraka yanayoambatana na unyanyasaji wa kijinsia ni kichocheo cha umasikini kinacholeta migongano na udhalilishaji unaopelekea kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa .

Hayo yamebainishwa mapema  na katibu wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA)Wilaya ya Manyoni mkoani Singida Bw.Saimon Boniphace Mtemi alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake.


Mbali na hayo alisema ,ni wajibu wa kila mtanzania kulipigia kelele suala la matumizi mabaya ya madaraka kwa kufanya juhudi ya kuwaelimisha wengine juu ya uwajibikaji utakaoleta amani kwenye jamii na kuepusha migongano inayoletwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Alisema,baadhi ya watu wenye dhamana wamekuwa wakiwanyanyasa wananchi pindi wanapohitaji huduma kiasi ambacho hupelekea kudai rushwa ya ngono na wakati mwingine kunyimwa huduma.

Pia aliseama mapambano dhidi ya rushwa ya ngono hayana uhuru na hivyo serikali kwa ujumla inapaswa kujipanga upya ili kuongeza ari ya mapambano dhidi ya rushwa .

Hata hivyo alisema wahanga wa rushwa ya ngono inapotokea wamedhalilishwa huwa hawajui ni wapi pa kukimbilia kwa kuogopa fedheha kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha na hivyo ni jukumu la watanzania waelewa kuwaelimisha.

Pamoja na hayo katibu huyo alibainisha kuwa matumizi mabaya ya madaraka ni kichocheo cha uvunjifu wa amani ambapo hutokea baada ya udhalilishaji na kusababisha matabaka mawili kutopana .

Hatua hii imekuja siku chache baada ya Tanzania kuazimisha siku ya amani duniani mkoani Dodoma ambapo jaji wa mahakama kuu ya Taifa Sofia Wambura alikiri kuwa rushwa ya ngono bado ipo na kwamba atakaedai au kutoa rushwa ya ngono wote watashitakiwa.

Aidha jaji wambura alitumia fursa hiyo kwa kusema kuwa yeyote atakaebainika kupata ajira bila kuwa na vigezo kwa kutoa rushwa sheria itachukua mkondo wake na kuwataka wananchi wote kuwa makini ili kuepuka suala la rushwa kwa maendeleo na kuitunza amani.


No comments:

Post a Comment