Waziri
wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akisalimiana na
watumishi wa kitupo cha afya cha mji mdogo wa Katoro.Waziri huyo amefika
katika kituo hicho ili kujionea hali ya
kituo hicho ambacho kinahudumia idadi kubwa ya wakazi wa mji huo pamoja na
jirani zake licha ya kuwa na changamoto ya watumishi pamoja na miundombinu
Monday, July 10, 2017
KIWANDA CHA MCHINA CHAFUNGIWA KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA
Katikati Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na
Mazingira Mhe. Luhaga Joelson Mpina (Mb.) akiongea na baadhi ya wananchi wa
mtaa wa Mivinjeni Buguruni Sukita Alipowatembelea kufuatia kero ya
utiririshwaji wa maji yanayosadikiwa kuwa na kemikali kutoka katika baadhi ya viwanda maji
yanayotumiwa na wakazi wa maeneo hayo kwa kumwagilia bustani za mboga mbonga. Kutoka
kulia kwake ni Naibu Meya wa wa Manispaa
ya Ilala Bw. Omary Kumbilamoto, Afisa Mazingira Ilala Bw. Adon Mapunda na
Diwani wa kata ya Buguruni Bw. Adam Fugane.
Friday, June 23, 2017
KUTOKA SHIMONI KABLA HUJAFA.
Watanzania wametakiwa kusimama katika zamu na nafasi zao ili
waweze kutolewa katika mashimo walikowekwa.
Kauli hiyo imetolewa na mwinjilisti wa kimataifa George
banali wakati akihubiri katika viwanja vya wapo mission International vilivyoko
mbezi Beach Jogoo jijini Dar es salaam,ambapo alisema kuwa njia pekee ya
mtanzania kufanikiwa kutoa katika shimo la mateso ni kumpa Yesu maisha yake.
Aidha alisema kuwa kutokana na watu wengi kuendelea kuteseka
na kutaabika njia moja tu ni kumpokea bwana Yesu kama Bwana na Mwokozi wa
maisha yako na hautaendeleea kukaa katika shimo.
Inawezekana shilo ulilowekwa ni shimo la mateso magonjwa na
shida mbalimbali pamoja na kuonewa na nguvu za giza sasa ni wakati wako wa
kufunguliwa na kuwekwa huru katika maisha yako.
Mukutano huo bado unaendelea ambapo waimbaji mbalimbali wa
nyimbo za injili wanahudumu kama vile Yes Kwaya,faraja Ntaboba,kikundi cha
kusifu na kuabudu cha BCIC na waimbaji wengine wengi.
Thursday, April 27, 2017
MIAKA 53 YA MUUNGANO; TUULINDE NA KUIMARISHA, TUPIGE VITA DAWA ZA KULEVYWA NA KUFANYA KAZI KWA BIDII
Kila mtanzania ametakiwa kuhakikisha anafanya jitihada za kuimarisha na kulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisiwa miaka 53 iliyopita.
Akizungumza leo wakati akihutubia wananchi katika sherehe za Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano katika uwanja wa Jamhuri uliopo mjini Dodoma, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alisema kuwa ni muhimu watanzania wakalinda Muungano kwa vile una manufaa kwa nchi zote mbili.
Friday, April 21, 2017
WIZARA YA ARDHI NA MAMLAKA YA MAPATO (TRA) WAENDESHA MAFUNZO YA KODI ZA PANGO YA ARDHI NA MAJENGO KWA WAANDISHI WA HABARI

Bw. Dennis Masami Mkuu wa Kitengo cha kodi Wizara ya Ardhi akitoa mada kwa wanahabari kwenye semina kuhusu Kodi za pango ya Ardhi na majengo iliyofanyika wizarani hapo ili kuwajegea uwezo wanahabari katika masuala ya sheria na taratibu za ulipaji wa kodi za pango ya Ardhi na kodi za majengo, Semina hiyo ambayo imeshirikisha pia wataalam wa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato (TRA) imefanyika leo jijini Dar es salaam ikishirikisha waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari pamoja na mitandao ya kijamii.
Subscribe to:
Posts (Atom)


