Showing posts with label BCIC Mbezi Beach. Show all posts
Showing posts with label BCIC Mbezi Beach. Show all posts

Friday, June 23, 2017

KUTOKA SHIMONI KABLA HUJAFA.

Watanzania wametakiwa kusimama katika zamu na nafasi zao ili waweze kutolewa katika mashimo walikowekwa.
Kauli hiyo imetolewa na mwinjilisti wa kimataifa George banali wakati akihubiri katika viwanja vya wapo mission International vilivyoko mbezi Beach Jogoo jijini Dar es salaam,ambapo alisema kuwa njia pekee ya mtanzania kufanikiwa kutoa katika shimo la mateso ni kumpa Yesu maisha yake.
Aidha alisema kuwa kutokana na watu wengi kuendelea kuteseka na kutaabika njia moja tu ni kumpokea bwana Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako na hautaendeleea kukaa katika shimo.
Inawezekana shilo ulilowekwa ni shimo la mateso magonjwa na shida mbalimbali pamoja na kuonewa na nguvu za giza sasa ni wakati wako wa kufunguliwa na kuwekwa huru katika maisha yako.
Mukutano huo bado unaendelea ambapo waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili wanahudumu kama vile Yes Kwaya,faraja Ntaboba,kikundi cha kusifu na kuabudu cha BCIC na waimbaji wengine wengi.

Wednesday, June 08, 2016

KAULI YA MWANGALIZI MKUU WA WAPO MISSION INTERNATIONAL WAKATI WA KUKUMBUKA SIKU YAKE YA KUZALIWA:


Tarehe 6 mwezi wa sita mwaka huu 2016 ni siku ya kumbukumbu ya  kuzaliwa kwa Askofu wa huduma ya BCIC na mwangalizi wa WAPO mission Askofu Sylivester Gamanywa, ambaye ameandika ujumbe ufuatao kwenye akaunti yake ya facebook.
SIKU NA MWEZI KAMA LEO NILIZALIWA DUNIANI!

Monday, March 28, 2016

SOMO: ROHO MTAKATIFU NA KARAMA ZAKE (3)

Askofu Sylvester Gamanywa, Mwangalizi Mkuu WAPO MIssion International. 
Wiki iliyopita tulifanya  uchambuzi wa fungu la karama za NGUVU ambazo ni karama ya Imani, Matendo ya miujiza na karama za kuponya magonjwa. Leo tunahitimisha kipengele hiki kwa kuchambua fungu la mwisho la karama za MAWASILIANO ambazo ni karama ya unabii, aina za lugha na tafsiri za lugha:
Tafsiri ya Karama ya unabii

Fungu la karama za mawasiliano ambazo ni “karama ya unabii”; “karama ya aina za lugha” na “karama ya tafsiri za lugha” Nitaanza na “karama ya unabii.” Kwanza kabla ya kutafsi karama tuanze na msamiati wa neno “unabii” kwa mujibu wa Biblia.  “unabii” ni ujumbe maalum kutoka kwa Mungu, ukiletwa na Roho Mtakatifu na kufunuliwa kwa mpokeaji/nabii/mtu aliyeteuliwa kwa wakati huo kuuwasilisha ujumbe huo kwa walengwa.

Ujumbe huu wa kinabii unapotangazwa na msemaji aliyeupokea, lazima uwasilishwe kwa lugha inayojulikana na wasikilizaji. Lazima ujumbe huo uwe umebeba taarifa ambazo mlengwa akiusikia atajitambua kuwa ujumbe huo ni wa kwakwe. Kwa maelezo mengine, unabii ni ujumbe wa Mungu kupitia kwa mpokeaji ili auwasilishe kwa walengwa pasipo yeye kuingiza mawazo yake ya kibinandamu.

Sasa tuje kwenye tafsiri ya “karama ya unabii”. Tafsiri nyepesi kueleweka kwa wazi zaidi ni “mpokeaji kupokea “zawadi ya kutumika kuwasilisha ujumbe kutoka kwa Mungu kwa ajili ya kuwajenga, kuwafariji na kuwatia moyo walengwa wa unabii huo; “Bali yeye ahutubuye, asema na watu maneno ya kuwajenga, kuwafariji, na kuwatia moyo.” (1 Kor.14:3)