Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha Dkt. Mahadhi Juma Maalim kuwa
Balozi wa Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha Kamishna wa Polisi Paul Amani
Moses Chagonja kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa KataviSaturday, January 30, 2016
MNADHIMU MKUU WA JWTZ,BALOZI WA TANZANIA KUWAIT,KATIBU TAWALA WA KATAVI NA MWANZA WAAPISHWA RASMI NA RAIS WA JAMHURI WA TANZANIA DKT JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI.
Friday, January 29, 2016
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO PROFESA MAKAME MBARAWA AKAGUA ATHARI ZA BARABARA MORO – DODOMA.
Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Morogoro Eng. Dorothy
Ntenga akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame
Mbarawa namna maji yanavyopiga kingo za daraja la Dumila wakati Waziri huyo
akikagua ujenzi wa kingo mpya zinazojengwa kudhibiti mafuriko hayo.
Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Dodoma Eng. Leornad
Chimagu (kulia),akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Profesa Makame Mbarawa kuhusu athari za mafuriko katika kingo za barabara ya
Gairo-Dodoma eneo la Kibaigwa mkoani Dodoma.
LHRC YAITAKA SERIKALI KUHESHIMU HAKI YA WATANZANIA KUPATA TAARIFA, YALAANI WABUNGE KUDHALILISHWA NA MBWA WA POLISI
Serikali imetakiwa kuheshimu haki ya kikatiba ya kuwapa wananchi
habari na taarifa muhimu zinazowahusu bila ya kujali gharama za taarifa hizo
kwa kuwa ni jukumu lake kufanya hivyo.
Thursday, January 28, 2016
SERIKALI YA TANZANIA KUAHIDI KUJENGA BARABARA KWA KIWANGO CHA LAMI.
Serikali imeahidi kuendelea na ujenzi
wa barabara katika maeneo tofauti nchini kwa kiwango cha lami ili kutatua adha
kubwa ya ubovu wa barabara ulipo katika maeneo mengi nchini.
Hayo yamesemwa leo Mjini Dodoma na
Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Eng Godwin
Ngonyani akijibu maswali ya wabunge waliouliza kuhusu mpango wa serikali
kuboresha barabara zilizopo na kujenga mpya ili kukabiliana na adha ya ubovu wa
barabara nchini.
WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO TAARIFA KWA UMMA.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO
TAARIFA KWA UMMA
KUFUNGWA KWA MUDA BARABARA YA MPANDA - KOGA - TABORA
Tunapenda kutoa taarifa kwa Umma kuwa, Barabara ya Mpanda - Koga - Tabora imefungwa kwa muda kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini zilizosababisha kufurika kwa mto Koga na kufanya daraja la Koga, lililopo mpakani mwa Mikoa ya Katavi na Tabora kutopitika na hivyo kukata mawasiliano ya barabara katika mikoa hiyo.
Kutokana na kukatika kwa mawasiliano ya barabara kupitia daraja hilo, tunaomba wananchi kusitisha safari kwa kutumia barabara hiyo ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza hadi hapo barabara hiyo itakapofunguliwa mara tu baada ya maji kupungua katika eneo hilo.
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imechukua hatua hiyo kwa mujibu wa Kifungu cha 41 (1) cha Sheria ya Barabara Na. 13 ya Mwaka 2007 na Kanuni ya 8 (1) ya Kanuni za Usimamizi za Barabara za Mwaka 2009.
Wizara, inaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza katika kipindi hiki chote.
Imetolewa na:
Eng. Joseph Nyamhanga
KATIBU MKUU (UJENZI)
28/01/2016
Tuesday, January 26, 2016
TRA YAOMBA USHIRIKIANO KUTOKA KWA WANANCHI.
Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA) yawaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa
za Maafisa wanaofanya kazi kinyume na maadili.
Akiongea
na mwandishi wa habari hii leo Jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Huduma na
Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo amesema kuwa TRA ina Idara Maalumu
ijulikanayo kama Idara ya Mambo ya Ndani ya TRA ambayo inashughulika na
kufuatilia maadili ya watumishi wa sekta hiyo nchi nzima.
Subscribe to:
Posts (Atom)





