Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA) yawaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa
za Maafisa wanaofanya kazi kinyume na maadili.
Akiongea
na mwandishi wa habari hii leo Jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Huduma na
Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo amesema kuwa TRA ina Idara Maalumu
ijulikanayo kama Idara ya Mambo ya Ndani ya TRA ambayo inashughulika na
kufuatilia maadili ya watumishi wa sekta hiyo nchi nzima.
