Showing posts with label Mkurugenzi Kayombo.. Show all posts
Showing posts with label Mkurugenzi Kayombo.. Show all posts

Tuesday, January 26, 2016

TRA YAOMBA USHIRIKIANO KUTOKA KWA WANANCHI.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yawaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za Maafisa wanaofanya kazi kinyume na maadili.

Akiongea na mwandishi wa habari hii leo Jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo amesema kuwa TRA ina Idara Maalumu ijulikanayo kama Idara ya Mambo ya Ndani ya TRA ambayo inashughulika na kufuatilia maadili ya watumishi wa sekta hiyo nchi nzima.