Showing posts with label barabara kkujengwa kwa kiwango cha lami. Show all posts
Showing posts with label barabara kkujengwa kwa kiwango cha lami. Show all posts

Thursday, January 28, 2016

SERIKALI YA TANZANIA KUAHIDI KUJENGA BARABARA KWA KIWANGO CHA LAMI.

Serikali imeahidi kuendelea na ujenzi wa barabara katika maeneo tofauti nchini kwa kiwango cha lami ili kutatua adha kubwa ya ubovu wa barabara ulipo katika maeneo mengi nchini.

Hayo yamesemwa leo Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano  Mhe. Eng Godwin Ngonyani akijibu maswali ya wabunge waliouliza kuhusu mpango wa serikali kuboresha barabara zilizopo na kujenga mpya ili kukabiliana na adha ya ubovu wa barabara nchini.