Serikali imeahidi kuendelea na ujenzi
wa barabara katika maeneo tofauti nchini kwa kiwango cha lami ili kutatua adha
kubwa ya ubovu wa barabara ulipo katika maeneo mengi nchini.
Hayo yamesemwa leo Mjini Dodoma na
Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Eng Godwin
Ngonyani akijibu maswali ya wabunge waliouliza kuhusu mpango wa serikali
kuboresha barabara zilizopo na kujenga mpya ili kukabiliana na adha ya ubovu wa
barabara nchini.