Anitha Jonas –
MAELEZO
Tarehe 23/05/2016
Dar es Salaam.
SERIKALI imesema kuwa
mtu yeyote atakayekamatwa kwa kosa la husisha au kushawishi mtoto kujiingiza
katika matumizi au biashara ya dawa za kulevya atahukumiwa kifungo cha miaka
isiyopungua 30.
Hayo yamesema na Mkuu
wa Kitengo cha Elimu, Habari na Takwimu wa Tume ya kuratibu na kudhibiti wa
Dawa za Kulevya, Amani Msami kupitia Taarifa ya tume hiyo kwa vyombo vya
habari.
Msami alisema adhabu
hiyo ni kwa mujibu wa Sheria ya kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya Na.5
ya mwaka 2015 tofauti na Sheria ya Kuzuian Biashara Haramu ya Dawa za Kulevya
Na. 9 ya mwaka 1995 iliyokuwa na mapungufu.