Monday, May 23, 2016

MWENYEKITI WA MTAA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI MWANZA.



































MWENYEKITI wa Mtaa wa Bulale wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Alphonce  Nyinzi  (48) ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiofahamika wakati akielekea nyumbani kwake.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa  Polisi Mkoa wa Mwanza, SACP Ahmed Msangi amesema kuwa tukio hilo lilitokea Aprili 22 mwaka  huu majira ya  saa 2 usiku.

SERIKALI KUENDELEA KUONGEZA BAJETI KWA AJILI YA BARABARA.

index

































Na Benedict Liweng, MAELEZO, Dodoma.
SERIKALI imesema itaendelea kuongeza bajeti kwa ajili ya barabara kadri uwezo wa kifedha utakavyoongezeka.
Hayo yamesemwa leo Bungeni Dodoma na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Miko na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jafo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum. Mhe. Sophia Mwakagenda aliyetaka kujua utayari wa Serikali katika kukubali ombi la Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, Mkoani Mbeya na kuongeza fedha katika Bajeti ya mwak 2016/2017.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI MKUU NA JAJI MKUU IKULU JIJINI DAR ES SALAAM,

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo na Rais Dkt. Magufuli.

WAZIRI MKUU KUHUDHURIA MKUTANO WA ADB ZAMBIA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa anaondoka nchini (Jumatatu, Mei 23, 2016) kwenda Lusaka, Zambia kuhudhuria Mkutano wa 51 wa Mwaka wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (51st Annual Meeting of the Board of Governors of the African Development Bank – AfDB) utakaofanyika kesho (Jumanne, Mei 24, 2016).

Waziri Mkuu anahudhuria mkutano huo kwa niaba ya Mheshimiwa Rais, Dk. John Pombe Magufuli.

ATAKEYEHUSISHA WATOTO NA DAWA ZA KULEVYA JELA MIAKA 30.

Anitha Jonas – MAELEZO
Tarehe 23/05/2016
Dar es Salaam.
SERIKALI imesema kuwa mtu yeyote atakayekamatwa kwa kosa la husisha au kushawishi mtoto kujiingiza katika matumizi au biashara ya dawa za kulevya atahukumiwa kifungo cha miaka isiyopungua 30.
Hayo yamesema na Mkuu wa Kitengo cha Elimu, Habari na Takwimu wa Tume ya kuratibu na kudhibiti wa Dawa za Kulevya, Amani Msami kupitia Taarifa ya tume hiyo kwa vyombo vya habari.
Msami alisema adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Sheria ya kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya Na.5 ya mwaka 2015 tofauti na Sheria ya Kuzuian Biashara Haramu ya Dawa za Kulevya Na. 9 ya mwaka 1995 iliyokuwa na mapungufu.

Saturday, May 21, 2016

RC PAUL MAKONDA AFUNGUA MACHINJIO YA VINGUNGUTI JIJINI DAR ES SALAAM

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi wakati alipowasili kuzungumza na wafanyabiashara wa nyama katika Machinjio ya Vingunguti kabla ya kuifungua rasmi jana. Katikati ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omari Kumbilamoto ambaye ni Diwani wa Kata ya Vingunguti.

MATUKIO YA PICHA BUNGENI DODOMA, JUMAMOSI 21 MEI, 2016

Mbunge wa CHADEMA, Mhe. Mwita Mwikwabe Waitara (kushoto) akiwa ameongozana na Mbunge mwenzie kuelekea ndani ya Bunge mjini Dodoma 21 Mei, 2016 kwa ajili ya vikao vya asubuhi siku ya Jumamosi bungeni hapo.
bu2Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Vangimembe Lukuvi akisoma Bajeti ya Wizara yake kwa Mwaka wa Fedha 2016/17 leo Bungeni mjini Dodoma 21 Mei, 2016.