Showing posts with label Amani Msami. Show all posts
Showing posts with label Amani Msami. Show all posts

Monday, May 23, 2016

ATAKEYEHUSISHA WATOTO NA DAWA ZA KULEVYA JELA MIAKA 30.

Anitha Jonas – MAELEZO
Tarehe 23/05/2016
Dar es Salaam.
SERIKALI imesema kuwa mtu yeyote atakayekamatwa kwa kosa la husisha au kushawishi mtoto kujiingiza katika matumizi au biashara ya dawa za kulevya atahukumiwa kifungo cha miaka isiyopungua 30.
Hayo yamesema na Mkuu wa Kitengo cha Elimu, Habari na Takwimu wa Tume ya kuratibu na kudhibiti wa Dawa za Kulevya, Amani Msami kupitia Taarifa ya tume hiyo kwa vyombo vya habari.
Msami alisema adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Sheria ya kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya Na.5 ya mwaka 2015 tofauti na Sheria ya Kuzuian Biashara Haramu ya Dawa za Kulevya Na. 9 ya mwaka 1995 iliyokuwa na mapungufu.