Showing posts with label waziri wa nchi. Show all posts
Showing posts with label waziri wa nchi. Show all posts

Friday, December 02, 2016

WANAWAKE WAONGOZA KUWA NA VIRUSI VYA UKIMWI NCHINI

Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Utafiti wa Viashiria vya Virusi vya UKIMWI (VVU) na Maralia (THMIS) wa mwaka 2011/2012 kwa upande wa Tanzania Bara vinaonyesha kuwa idadi kubwa ya wanawake wameambukizwa ugonjwa huo kuliko wanaume.

Thursday, July 14, 2016

JK - UTAFITI WA KINA WAHITAJIKA KATIKA KUKUMBANA NA MABADILIKO YA TABIA NCHI AFRIKA


Rais mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akifungua mkutano wa tatu wa Sera za Mabadiliko ya Tabia Nchi jijini Dar es Salaam iliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Climate Strategies. Mkutano huo ilijumuisha watafiti na watunga sera 80 kutoka nchi zaidi ya 10 nje na ndani ya Afrika chini ya kauli mbiu "Kutekeleza Makubaliano ya Paris - Suluhu Mpya za Utafiti kwa ajili ya Nchi zinazoendelea." Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa mkutano huo Bw. Chuks Okereke, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano Mhe. January Makamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja.

JK - UTAFITI WA KINA WAHITAJIKA KATIKA KUKUMBANA NA MABADILIKO YA TABIA NCHI AFRIKA


Rais mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akifungua mkutano wa tatu wa Sera za Mabadiliko ya Tabia Nchi jijini Dar es Salaam iliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Climate Strategies. Mkutano huo ilijumuisha watafiti na watunga sera 80 kutoka nchi zaidi ya 10 nje na ndani ya Afrika chini ya kauli mbiu "Kutekeleza Makubaliano ya Paris - Suluhu Mpya za Utafiti kwa ajili ya Nchi zinazoendelea." Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa mkutano huo Bw. Chuks Okereke, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano Mhe. January Makamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja.

Thursday, May 19, 2016

MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI, DODOMA.

Waziri wa Nishati na Mdini, Mhe. Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi mara walipokutana Bungeni mjini Dodoma wakati wa Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madinileo 19 Me, 2016 bungeni hapo. 

Friday, March 18, 2016

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA YATEMBELEA TASAF NA TUME YA UTUMISHI WA UMMA:

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Mendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Ladislaus Mwamanga akiwasilisha mada ofisini kwake wakati wa kikao na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akitoa mchango wake wakati wa kikao kati ya Tume ya Utumishi wa Umma na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa . 

Thursday, January 07, 2016

WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS TAMISEMI MHE. GEORGE SIMBACHAWENE (MB) AMEMUAGIZA MKURUGENZI WA MANISPAA YA ILALA KUMSIMAMISHA KAZI KAIMU AFISA BIASHARA WA MANISPAA YA ILALA BW. DENNIS. N. MREMA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. George Simbachawene (Mb) amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kumsimamisha kazi mara moja Kaimu Afisa Biashara wa Manispaa ya Ilala Bw. Dennis. N. Mrema kuanzia leo tarehe 07 Januari, 2016 kwa kosa la kusababisha upotevu wa Mapato ya Serikali kutokana na urasimu wa kukusudia, mazingira ya rushwa na uzembe katika utoaji wa leseni za Biashara.

Kutokana na hali hiyo Mhe. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI ameelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kumuondoa kwenye nafasi yake Kaimu Afisa Biashara wa Manispaa ya Ilala na nafasi yake kukaimiwa na mtu mwingine ili kupisha uchunguzi zaidi juu ya tuhuma zilizotolewa dhidi yake.

Mhe. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais –TAMISEMI amefikia uamuzi huu baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa Wafanyabiashara ambao wamemlalamikia Mtendaji huyu kwa ukiukwaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu za utoaji wa Leseni za Biashara, Urasimu na Mazingira ya rushwa.