Showing posts with label Dodoma. Show all posts
Showing posts with label Dodoma. Show all posts

Friday, April 29, 2016

RAIS DKT. JOHN MAGUFULI AWASILI MKOANI DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma wakati akitokea mjini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana.

Thursday, January 21, 2016

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMESEMA KUWA WANANCHI WANAANGALIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) MAANA NDIYO KITOVU CHA NCHI.


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ndiyo kitovu cha nchi na kwamba kila Mtanzania ameelekeza jicho lake pale kwa sababu anasubiri kupata huduma ya msingi.

“Hapa ndiyo kitovu cha nchi na Watanzania wote macho yao yako huku. Kwa nini? Kwa sababu huduma zinasowagusa za barabara, maji, elimu, zinatokea huku kwa maana ya bajeti na usimamizi,” alisema.

Ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Januari 21, 2016) wakati akizungumza na wakurugenzi, wakuu wa taasisi na watumishi wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwenye mkutano uliofanyika ofisi ya TAMISEMI mjini Dodoma.