Frank
Mvungi
Mahakama
ya Wilaya ya Chato Mkoani Geita imemtia hatiani Mgambo wa Mahakama ya mwanzo
Buseresere Bw. Majaliwa Revelian Gwakilala kwa makosa ya kuomba na kupokea
Rushwa kinyume na kifungu cha
15 (1 na 2) cha
Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
Kwa
Mujibu wa Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Taasisi ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kesi dhidi ya Mtuhumiwa huyo ilifunguliwa mnamo
tarehe 14/1/2016.
Akisoma
hukumu mbele ya mwendesha mashitaka wa TAKUKURU Augustino Mtaki, Hakimu Hakimu
Mfawidhi wa Wilaya hiyo Mh. Mh. Jovith Kato alisema kuwa ushahidi
uliowasilishwa mahakamani hapo na upande wa mwendesha Mashitaka umethibitisha
pasipo shaka yoyote kuwa Mtuhumiwa alitenda kosa hilo.



