Showing posts with label Rushwa. Show all posts
Showing posts with label Rushwa. Show all posts

Friday, May 27, 2016

VITA YA RUSHWA SI NGUVU YA SODA - WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema vita inayoendeshwa na Serikali ya awamu ya tano dhidi ya wala rushwa na wale wanaofanya ufisadi siyo nguvu ya soda kama wengi wanavyofikiri.
“Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kupambana na wala rushwa na mafisadi. Wala hatutanii. Hawa tutacheza nao na wala wasidhani vita hii ni nguvu ya soda. Tutaendelea kuwasaka hadi tufike mwisho,” alisema Waziri Mkuu wakati akizungumza na Watanzania waishio Zambia katika mkutano uliofanyika kwenye Ubalozi wa Tanzania jijini Lusaka, Zambia juzi jioni (Jumanne, Mei 24, 2016).

Tuesday, March 01, 2016

SHILINGI LAKI MOJA YAMPONZA DAKTARI WA HOSPITALI YA LIGULA AMBAYO NI YA MKOA WA MTWARA.

Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Waganga, Wauguzi na wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara wakati alipoitembelea Februari 29, 2016.

·         Ni baada ya kudai rushwa ya sh. 100,000/- kumfanyia upasuaji mgonjwa.
·         Mama alilazimika kuuza shamba ili apate fedha za kumtibia baba yake
·         Aagiza maduka ya dawa nje ya hospitali hiyo yafungwe leo hii
·         Amwagiza RAS aitishe kikao cha watumishi wote leo saa 9 alasiri
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza kusimamishwa kazi kwa Dk. Fortunatus Namahala wa kitengo cha upasuaji katika hospitali ya Ligula ambayo ni hospitali mkoa wa Mtwara kutokana na tuhuma za kumdai mgonjwa rushwa ya sh. 100,000/-.