Showing posts with label Dk. Shaibu Maarifa.. Show all posts
Showing posts with label Dk. Shaibu Maarifa.. Show all posts

Tuesday, March 01, 2016

SHILINGI LAKI MOJA YAMPONZA DAKTARI WA HOSPITALI YA LIGULA AMBAYO NI YA MKOA WA MTWARA.

Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Waganga, Wauguzi na wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara wakati alipoitembelea Februari 29, 2016.

·         Ni baada ya kudai rushwa ya sh. 100,000/- kumfanyia upasuaji mgonjwa.
·         Mama alilazimika kuuza shamba ili apate fedha za kumtibia baba yake
·         Aagiza maduka ya dawa nje ya hospitali hiyo yafungwe leo hii
·         Amwagiza RAS aitishe kikao cha watumishi wote leo saa 9 alasiri
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza kusimamishwa kazi kwa Dk. Fortunatus Namahala wa kitengo cha upasuaji katika hospitali ya Ligula ambayo ni hospitali mkoa wa Mtwara kutokana na tuhuma za kumdai mgonjwa rushwa ya sh. 100,000/-.