Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Waganga, Wauguzi na
wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara wakati alipoitembelea Februari 29,
2016.
·
Ni baada ya kudai rushwa ya sh. 100,000/- kumfanyia
upasuaji mgonjwa.
·
Mama alilazimika kuuza shamba ili apate fedha za
kumtibia baba yake
·
Aagiza maduka ya dawa nje ya hospitali hiyo yafungwe
leo hii
·
Amwagiza RAS aitishe kikao cha watumishi wote leo
saa 9 alasiri
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza kusimamishwa kazi kwa Dk. Fortunatus
Namahala wa kitengo cha upasuaji katika hospitali ya Ligula ambayo ni hospitali
mkoa wa Mtwara kutokana na tuhuma za kumdai mgonjwa rushwa ya sh. 100,000/-.