Showing posts with label NEC. Show all posts
Showing posts with label NEC. Show all posts

Saturday, March 19, 2016

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) HAITAMBUI KUJITOA KWA MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KIJITOUPELE ZANZIBAR

Na Clarence Nanyaro- NEC
Tume  ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),imesema haitambui  kujitoa kwa Chama cha Wananchi (CUF),katika uchaguzi wa Mbunge  Jimbo la Kijitoupele hapa Zanzibar unaotarajiwa kufanyika Jumapili licha ya kuwa  Tume imepokea barua rasmi toka kwa uongozi wa Chama hicho.
Mkurugenzi wa uchaguzi wa Tume ya Taifa Bw Kailima Ramadhani amesema Tume imefikia maamuzi hayo kutokana na ukweli kuwa barua hiyo ya CUF imechelewa huku maandalizi ya uchaguzi huo yakiwa yamekamilika na ni Wananchi tu kwa sasa Wanasubiriwa kwenda kupiga kura.

Wednesday, January 20, 2016

MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA NEC LIMEFUNGULIWA NA MWENYEKITI WA TUME HIYO JAJI DAMIAN LUBUVA

 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mhe. Jaji Mstaafu Damian Lubuva (kushoto) ambaye ni mgeni rasmi wa mkutano huo, akiongea na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa NEC (hawapo pichani) leo katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam kuhusu masuala ya maadili na na ufanisi kazini.
Mkurugenzi wa Uchaguzi, Bwana Ramadhani Kailima akiongea na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa NEC (hawapo pichani) leo katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam kuhusu masuala ya maadili na na ufanisi kazini kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi.