Showing posts with label Mchungaji Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’. Show all posts
Showing posts with label Mchungaji Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’. Show all posts

Monday, December 05, 2016

SEMENI LIKUNYWA POMBE GANI NA SEHEMU GANI

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’ baada ya kudaiwa kumfanyia fujo jirani yake ameendelea kujibu madai hayo kwa mtindo wa ‘kudonoa donoa’ na jana aliwataka wanaodai kuwa alilewa siku hiyo wataje alikunywa pombe gani na katika baa gani. 

Wiki mbili zilizopita, taarifa kwenye vyombo vya habari zilisema kwamba Mchungaji Lusekelo alikwaruzana na majirani zake huku akidaiwa kuwa alikuwa amelewa jambo ambalo lilifanya achukuliwe na kuhojiwa na polisi. 

Monday, June 06, 2016

RAIS DKT. MAGUFULI AHUDHURIA IBADA KANISA LA MAOMBEZI LA MCHUNGAJI ANTONY LUSEKELO ‘MZEE WA UPAKO’ UBUNGO KIBANGU

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo wakati akiagana na Mchungaji Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’ katika kanisa lake la Maombezi lililopo Ubungo Kibangu jijini Dar es Salaam. Rais Dkt. Magufuli alihudhuria ibada hiyo pamoja na kukagua barabara inayotoka Ubungo Kibangu hadi Barabara ya Mandela eneo la Riverside.