Showing posts with label mkuu wa idara ya huduma ya wagonjwawa nje. Show all posts
Showing posts with label mkuu wa idara ya huduma ya wagonjwawa nje. Show all posts

Thursday, January 21, 2016

HUDUMA ZA WAGONJWA WA NJE KUBORESHWA KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI.

Na Anaseli Stanley,
Hospital ya Taifa ya Muhimbili imeboresha huduma za afya kwa wagonjwa wa nje ili kusaidia wagonjwa kupata Huduma kwa wakati pamoja na kupunguza msongamano  katika  eneo moja ndani ya hospital hiyo.
Hayo yameelezwa jijini Dar es salaam Na Mkuu wa idara ya Huduma ya wagonjwa wa nje Dr. Raymond Mwenesano ambapo amesema kuwa wagonjwa watapata muda zaidi wa kutibiwa na kupata ushauri wa madaktali bingwa katika kliniki mbalimbali ambapo awali kliniki zilikuwa hazitoi Huduma kwa kiwango kisichoridhisha kutokana na kutokuwepo kwa muda wa kutosha.