Na Anaseli Stanley,
Hospital ya Taifa ya Muhimbili
imeboresha huduma za afya kwa wagonjwa wa nje ili kusaidia wagonjwa kupata
Huduma kwa wakati pamoja na kupunguza msongamano katika eneo moja
ndani ya hospital hiyo.
Hayo
yameelezwa jijini Dar es salaam Na Mkuu wa idara ya Huduma ya wagonjwa wa nje
Dr. Raymond Mwenesano ambapo amesema kuwa wagonjwa watapata muda zaidi wa kutibiwa na kupata ushauri wa madaktali bingwa katika kliniki mbalimbali ambapo
awali kliniki zilikuwa hazitoi Huduma kwa kiwango kisichoridhisha kutokana na
kutokuwepo kwa muda wa kutosha.