ARDHI KUKUSANYA BILIONI 111.77 MWAKA UJAO WA FEDHA.
Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi inatarajia kukusanya shilini bilioni 111.77 kutokana na vyanzo mbalimbali za shughuli za sekta za ardhi katika mwaka ujao wa fedha.
Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi wakati akiwasilisha bungeni hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka ujao wa fedha.
Alisema kuwa mapato hayo yanatarajiwa kupatikana kutokana upimamaji na ukutoaji hatimiliki za viwanja na mashamba 400,000 kwa wananchi.