SHIRIKA LA Majisafi na Majitaka Dar es salaam
(DAWASCO), imetangaza kuwapo tatizo la upatikanaji wa huduma ya Maji katika
maeneo yote yanayohudumiwa na mtambo wa Ruvu chini ya jiji la Dar es salaam,
pamoja na baadhi ya maeneo ya mji wa Bagamoyo mkoani Pwani kutokana
na mtambo huo kuzimwa kwa wastani wa saa 48 kuanzia siku ya Jumamosi 23/01/2016
hadi Jumapili 24/01/2016.
