Muungano mkuu wa upinzani nchini Jamhuri ya Demokrasia ya Congo unasema kuwa zaidi ya watu 50 waliuawa wakati wa mandamano ya kumpinga rais Joseph Kabila siku ya Jumatatu mjini Kinshasa.
Mmoja wa walioshuhudia anasema polisi waliwafyatulia risasi waandamanaji.