Mkurugenzi
wa mashtaka Tanzania DPP Biswalo Mganga amemfuata Kitilya na wenzake katika
mahakama ya Rufani ambapo ameongoza jopo la mawakili watano kutoka Jamuhuri na
kuiomba mahakama ya rufani kutengua uamuzi
uliotolewa na mahakama kuu na iamuru mahakama kuu kusikiliza rufani
hiyo.
Rufaa hiyo
imesikilizwa na mahakama ya rufani Tanzania mbele ya majaji wa tatu Salim Masati,Agustin Mwarinja na Musa kipenga,ambapo wamesikiliza hoja za
pande zote mbili pasipo kutoa maamuzi .