KAMANDA wa polisi
mkoani Pwani, Boniventure Mushongi, akizungumzia tukio la mauaji
lililotokea wilayani Kibiti mkoani Pwani.
Watu watatu wamepoteza
maisha mmoja kati yao akiwa OC CID Kibiti baada ya kuuwawa na kundi la
watu wanaodhaniwa ni majambazi wakiwa na silaha aina ya SMG/SAR huko
eneo la Jaribu Mpakani kata ya Majawa ,Kibiti .
Tukio hilo limetokea
feb 21 majira ya saa mbili usiku ambapo watu sita walivamia katika
kituo cha ukaguzi wa mazao ya misitu na kuuwa watu watatu .
Kamanda wa polisi
mkoani Pwani,Boniventure Mushongi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo
,aliwataja waliouawa kuwa ni OC CID wilaya ya Kibiti sp.Peter Kubezya
ambae amepigwa risasi kwenye kiuno .
Wengine ni Peter
Kitundu Mkaguzi wa maliasili kituo cha Jaribu Mpakani na mgambo
aliyekuwa akifanyakazi za ulinzi kwenye kizuizi hicho, Athumani Ngambo .
Kamanda Mushongi alisema wote hao wawili waliuawa kwa kupigwa risasi kichwani na begani na kupoteza maisha papo hapo .
Aidha wakati majambazi
hayo yakifanya uhalifu huo waliweza kuwaita wananchi wafike kwenye
kizuizi hicho ili wachukue mkaa na mazao ya misitu .
Kufuatia wito huo wananchi walijitokeza na kwenda kujibebea mkaa na mazao hayo kisha kuondoka nayo.
“Baada ya kutokea kwa
tukio hilo kundi la makachero likiongozwa na OC CID Kubezya lilifika
eneo la tukio kupambana na wahalifu lakini wakiwa kwenye majibizano ya
kurushiana risasi mkuu huyo wa upelelezi alijeruhiwa kiunoni ambapo
alifariki akiwa njiani akielekea hospitali ya mission ya Mchukwi ”
alieleza Mushongi .
Kamanda Mushongi
alifafanua kwamba katika eneo la tukio kulikutwa pikipiki mbili namba
MC 853 AHH aina ya Toyo na MC 799 aina ya Sunlg pamoja na kipeperushi
chenye ujumbe wa kitisho .
Kutoka vyanzo
mbalimbali huko Kibiti vinasema vipeperushi hivyo vinaeleza kupinga
kuwepo kwa vizuizu vya mazao ya misitu wilayani humo.
No comments:
Post a Comment