Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (mwenye suti ya kijivu anayenyoosha mkono)
akiwaeleza Waandishi wa Habari (hawapo pichani) juu ya Uamuzi wa Serikali wa
kulifuta Gazeti la MAWIO katika Daftari la Msajili wa Magazeti mara alipokutana
na waandishi hao 17 Januari 2016 katika Ukumbi wa Idara ya Habari uliopo jijini
Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari, Bw. Assah Mwambene, wa
pili kulia ni Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia usajili wa Magazeti, Bw.
Raphael Hokororo na anayemfuatia ni Mwanasheria wa Wizara Bw. Patrick Kipangula
