Na Daudi Manongi-MAELEZO
Viongozi wa umoja na wadau wa maendeleo wilaya
mpya ya kibiti (UWAWAMAKI) mkoani Pwani umepanga kufanya kongamano la kuunga
mkono tamko la Serikali ya awamu ya Tano ya Mhe.John Pombe Magufuli kwa
kuifanya Kibiti kuwa Miongoni mwa Wilaya mpya siku ya jumapili tarehe 29 saa
nne asubuhi kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari TEDEO Temeke jijini Dar es
Salaam.
Akiongea na waandishi wa Habari jijini Dar es
Salaam Katibu wa umoja huo Bw.Selemani Ndumbogani amesema kuwa wanakibiti wamefarijika sana na
kauli ya Serikali ya Kuipatia Kibiti wilaya jambo ambalo lilikuwa kilio cha
muda mrefu ikiwa ni takribani zaidi ya miaka arobaini tangu uhuru na kuongezea
kuwa walikuwa mbali sana na huduma muhimu za Serikali.