Showing posts with label TEDEO. Show all posts
Showing posts with label TEDEO. Show all posts

Friday, May 27, 2016

KIBITI KUFANYA KONGAMANO LA KUIPOKEA WILAYA MPYA KWA KUSHIRIKI SHUGHULI MBALIMBALI ZA MAENDELEO.

Na Daudi Manongi-MAELEZO

Viongozi wa umoja na wadau wa maendeleo wilaya mpya ya kibiti (UWAWAMAKI) mkoani Pwani umepanga kufanya kongamano la kuunga mkono tamko la Serikali ya awamu ya Tano ya Mhe.John Pombe Magufuli kwa kuifanya Kibiti kuwa Miongoni mwa Wilaya mpya siku ya jumapili tarehe 29 saa nne asubuhi kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari TEDEO Temeke jijini Dar es Salaam.
Akiongea na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Katibu wa umoja huo Bw.Selemani Ndumbogani  amesema kuwa wanakibiti wamefarijika sana na kauli ya Serikali ya Kuipatia Kibiti wilaya jambo ambalo lilikuwa kilio cha muda mrefu ikiwa ni takribani zaidi ya miaka arobaini tangu uhuru na kuongezea kuwa walikuwa mbali sana na huduma muhimu za Serikali.