Showing posts with label Profesa Tunus Mgaya. Show all posts
Showing posts with label Profesa Tunus Mgaya. Show all posts

Tuesday, May 31, 2016

KATIBU MTENDAJI WA TUME YA VYUO VIKUU (TCU) PROFESA TUNUS MGAYA ALIYESIMAMISHWA KAZI NA WAZIRI WA ELIMU AFUNGUKA MAMBO MAZITO

ALIYEKUWA Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Profesa Tunus Mgaya amesema amesikitishwa na taarifa zilizoandikwa katika vyombo vya habari za kukosoa maamuzi ya serikali ya kuwasimamisha kazi kuwa hayakuzingatia sheria na kanuni zilizowekwa.

Mgaya ambaye hakuwa tayari kueleza kama taratibu za kusimamishwa kwao zilifuata utaratibu au la, amewataka waandishi wa habari kuwa na vyanzo vya uhakika katika habari zao.