Showing posts with label Papa Francis. Show all posts
Showing posts with label Papa Francis. Show all posts

Tuesday, May 24, 2016

PAPA FRANCIS AKUTANA NA WAISLAMU MISRI

Image captionPapa Francis akikutana na kiongozi mkuu wa chuo kikuu cha kiislamu nchni Misri Al-Azhar
Kiongozi mmoja wa kidini nchini Misri amefanya mazungumzo na Papa Francis ,ikiwa ni ishara za hivi karibuni za kutaka kuimarisha uhusiano kati ya dini hizi mbili kubwa duniani.
''Mkutano huu ndio ujumbe'', Papa Francis alisema,huku akikutana na Sheik Ahmed el-Tayyib ,mkuu wa chuo kikuu cha kiislamu cha Al-Azhar na Msikiti.

Saturday, May 14, 2016

MJADALA WA WANAWAKE MASHEMASI WARUHUSIWA NA PAPA

Papa Francis akiwa Vatican.

Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, amesema ataunda tume itakayochunguza na kujadili uwezekano wa wanawake kuteuliwa kuwa mashemasi katika Kanisa hilo katika pendekezo linaloashiria uwazi wa kuruhusu wanawake kuteuliwa kuhudumu katika nafasi ambazo zimekuwa za wanaume pekee. Wazo hilo tayari limeanza kuibua hisia mbalimbali.