Showing posts with label Ortukai na Esilalei na Taasisi ya Tanzania Land Conservation Trust (TLCT). Show all posts
Showing posts with label Ortukai na Esilalei na Taasisi ya Tanzania Land Conservation Trust (TLCT). Show all posts

Tuesday, December 06, 2016

WAZIRI MKUU AMALIZA MGOGORO WA SHAMBA LA MANYARA RANCH KWA KUKABIDHI HATI KWA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MONDULI,

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemaliza mgogoro wa ardhi  uliodumu kwa miaka 17 kati ya vijiji viwili vya Ortukai na Esilalei na Taasisi ya Tanzania Land Conservation Trust (TLCT) baada ya kukabidhi hati ya  shamba la Manyara Ranch  kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, Stephen Ulaya.
Hati hiyo imetolewa jana jioni (Jumapili, Desemba 4, 2016) na Waziri Mkuu katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kata ya Mto wa Mbu kwenye viwanja vya Barafu baada ya kubadilishwa umiliki wa shamba hilo kwenda kwa wananchi wa vijiji  hivyo vilivyopo kwenye  Kata ya Elesilalei Wilayani Monduli Mkoani Arusha.