Na Beatrice Lyimo - MAELEZO
Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam Issaya Mwita ameiomba shirikisho la Michezo wa mpira wa miguu nchini (TFF) kuendelea kusimamia ligi kwa ustadi kulingana na ratibu na taratibu za mpira wa miguu kama zililivyoanishwa na Shirikisho la Soka Duniani( FIFA) pamoja na Shirikisho la Soka Barani Africa (CAF).
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyosainiwa Mstahiki Meya huyo inasema kuwa TFF inatakiwa kusimamia ligi hiyo ili kuainisha, kubainisha, kutajirisha na hatimae kutatua changamoto husika na kuwa na kiwango stahiki katika msimu unaofuata ukilinganisha na changamoto zilizojitokeza katika msimu uliopita.