Showing posts with label Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam Issaya Mwita. Show all posts
Showing posts with label Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam Issaya Mwita. Show all posts

Tuesday, May 17, 2016

MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA DAR ES SALAAM AMEIOMBA TFF KUSIMAMIA LIGU KWA USTADI KULINGANA NA TARATIBU ZA MPIRA WA MIGUU

Na Beatrice Lyimo - MAELEZO

Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam Issaya Mwita ameiomba shirikisho la Michezo wa mpira wa miguu nchini (TFF) kuendelea kusimamia ligi kwa ustadi kulingana na ratibu na taratibu za mpira wa miguu kama zililivyoanishwa na Shirikisho la Soka Duniani( FIFA) pamoja na Shirikisho la Soka Barani Africa (CAF).

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyosainiwa Mstahiki Meya huyo inasema kuwa TFF inatakiwa kusimamia ligi hiyo ili kuainisha, kubainisha, kutajirisha na hatimae kutatua changamoto husika na kuwa na kiwango stahiki katika msimu unaofuata ukilinganisha na changamoto zilizojitokeza katika msimu uliopita.