Showing posts with label Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii. Show all posts
Showing posts with label Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii. Show all posts

Friday, April 29, 2016

CHANJO YATOLEWA KWA WATOTO CHINI UUA MIAKA MITANO KUPUNGUZA VIFO VYA WATOTO:

Na Magreth Kinabo- Maelezo

Jamii imeshauriwa  kuwapeleka watoto wote wanaostahili kupata chanjo    walio chini ya umri wa miaka mitano katika vituo vya afya ili waweze kupatiwa chanjo  ili kuweza kutokomeza maradhi na kupunguza vifo vya watoto.
Kauli hiyo ilitolewa Aprili 27, mwaka huu na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Mpoki Ulisubisye wakati wa maadhimisho ya wiki ya chanjo nchini yaliyofanyika  kwenye hoteli ya Serena Jijini Dares Salaam.
Alisema  utoaji wa chanjo hiyo umeaanza Aprili 25 hadi 29 mwaka huu na  kaulimbiu ya mwaka huu ni ‘ Kumilisha Chanjo,Epuka Ugonjwa wa Polio’. Hivyo  vituo  vya  kutolea huduma za afya vinafunguliwa kuanzia saa 2: 00  asubuhi hadi saa 11.00 jioni.
“ Kila mmoja wetu anawajibu wa kuhakikisha  mtoto wake , mtoto wajirani au mlengwa mwingine yeyote anapewa haki ya chanjo ili kumzuia asipatwe na maradhi ambayo yanakingwa na chanjo au asiwe na hatari kwa wengine kwa kuwaletea ugonjwa,” alisema Dkt. Ulisubisye.