Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (katikati), ambaye mchana huu Rais Dk.John Magufuli amemteua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa jengo la upasuaji katika Hospitali ya Mwananyamala Dar es Salaam leo, ambalo litakuwa maalumu kwa ajili ya utoaji wa huduma za upasuaji kwa wajawazito na wagonjwa wengine wadharura. Kutoka kulia ni Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Azizi Msuya, Mwakilishi wa Kampuni ya GSM, Deogratias Ndejembi ambao watajenga jengo hilo na kushoto ni Mhandisi, Hersi Said kutoka GSM ambaye atasimamia ujenzi wa jengo hilo.
Mwakilishi wa Kampuni ya GSM Foundation, Deogratias Ndejembi akizungumza na wanahabari kuhusu ufadhili wao wa ujenzi wa jengo hilo.