Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imesema imeanza kupokea malipo kutoka kwa wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu wa miaka ya nyuma.
Wadaiwa hao wameibuka ikiwa ni siku saba tu, tangu bodi hiyo itangaze kiama kwa wadaiwa wote sugu wa walionufaika na mikopo ya bodi hiyo, ikiwa ni pamoja na kuanza kuchapisha majina na picha za wadaiwa hao kwenye vyombo vya habari, sambamba na kuunda tume ya kuwasaka wadai hao.