Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeamua kulifungia kwa miezi 36 gazeti la “MSETO”. Amri ya kulifungia Gazeti hilo imetolewa kwa Tangazo la Serikali Na. 242 lililotolewa tarehe 10 Agosti, 2016. Uamuzi huo umetolewa kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976 Sura ya 229, kifungu 25(1).
