Showing posts with label James Mbatia. Show all posts
Showing posts with label James Mbatia. Show all posts

Thursday, July 21, 2016

NCCR wamtimua makamu Mwenyekiti wa Chama

Chama cha NCCR – Mageuzi kimemvua uanachama makamu mwenyekiti wake (Bara), Leticia Ghati (pichani) kikimtuhumu kujihusisha na migogoro ndani ya chama na tuhuma nyingine za kijinai. 

Friday, June 10, 2016

UKAWA WAMJIBU NAIBU SPIKA WAMWAMBIA POSHO AKAWATISHIE WATOTO.


Siku mbili baada ya Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson kuagiza wabunge wa upinzani wanaoingia Bungeni na kisha kuondoka wakisusa vikao wasilipwe posho, wabunge hao wamejibu wakiubeza na kuupinga uamuzi huo.

Wakiongea kwa nyakati tofauti, wabunge wa upinzani wamekosoa uamuzi huo wakieleza kuwa Dk. Tulia alihukumu kesi inayomhusu, kitendo walichosema sio haki.