Wakati jeshi la polisi likisema linajiimarisha, vitendo vya ujambazi vinazidi kuitikisa nchi baada ya kundi la watu wasiojulikana kuvamia ofisi za Kampuni ya Ahsante Tours ya mjini Moshi, kuua walinzi wawili na kuiba Sh 65.5milioni.
Tukio hilo limekuja siku chache baada ya watu wasiojulikana kuvunja duka la kubadilisha fedha la Chase Forex Bureau De Change la mjini Moshi na kuiba zaidi ya Sh120 milioni.
